Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 95 2023-09-06

Name

Mbarouk Juma Khatib

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbwini

Primary Question

MHE. MBAROUK JUMA KHATIBU aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi katika eneo ambalo linajengwa Bandari Kuu ya mizigo Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbarouk Juma Khatibu, Mbunge wa Jimbo la Bumbwini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya Bandari ambayo imejenga bandari ya mizigo eneo la Manga Pwani – Zanzibar imetenga eneo na imeandaa michoro kwa ajili ya kujenga ofisi zitakazotumiwa na vyombo vya ulinzi na usalama kikiwemo kituo cha polisi, ninakushukuru.