Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 98 2023-09-06

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, Serikali inatambua gunia kuwa kipimo au kifungashio kwa mujibu wa Sheria?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo, The Weights and Measures Act (Amendment) Order, G.N. No. 725 of 2018, jedwali la 10 chini ya kifungu cha 2(b) cha Jedwali hilo ambacho kinasema mazao ya mashambani yatafungashwa kwa uzito usiozidi kilogramu 100. Pamoja na kuelekeza wauzaji au wanunuzi wa mazao kutumia mizani, Serikali haitambui gunia kuwa kipimo bali ni kifungashio.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo nitoe wito kwa wadau wote kuepuka matumizi ya gunia kama kipimo kwani kwa kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Vipimo, nakushukuru.