Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 101 2023-09-06

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami Barabara ya Simbo hadi Ilagala?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kutambua umuhimu wa barabara ya Simbo – Ilagala – Kalya yenye urefu wa kilometa 234 imeanza kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Daraja la Lower Malagarasi ambalo lipo katika barabara hii na kazi zinatarajiwa kukamilika Disemba, 2023. Kuhusu usanifu wa barabara hiyo, Serikali imeanza kutenga fedha kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambapo katika mwaka wa fedha 2023/2024, Mheshimiwa Mbunge tumemtengea shilingi milioni 100 ili kufanya kazi hiyo.