Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 103 2023-09-06

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-

Je, Tanzania ina Madaktari Bingwa Wazalendo wa magonjwa ya binadamu wangapi na katika magonjwa gani?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adamu Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa Tanzania ina jumla ya Madaktari Bingwa Wazalendo 2,469 ambao wamesajiliwa na Baraza la Madaktari Tanganyika kwa fani mbalimbali za Udaktari Bingwa. Kati yao Madaktari Bingwa 2,098 wapo katika Sekta ya Umma na Madaktari Bingwa 371 wapo Sekta Binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Madaktari hawa wamegawanyika katika maeneo 28 ya Ubingwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.