Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 106 2023-09-06

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani kuhakikisha wazee waliopigana Vita ya Pili ya Dunia chini ya Chama cha TLC wananufaika na mali zao?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silyvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwezi Julai, 2022, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa iliunda Kamati maalum ya kuchambua na kutoa ushauri kuhusu hatma ya Askari waliopigana Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka 1939 – 1945 na kuhusu mali za Chama cha Tanzania Legion & Clubs (TLC).

Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini hiyo ilibaini kuwa Askari waliopigana Vita Kuu ya Dunia walikuwa 737, kati yao 57 wapo hai na 680 wamekwishafariki. Tathmini ilionesha pia kuwa TCL inazo mali zenye thamani ya Shilingi 37,366,323,048.000. Hata hivyo, baadhi ya mali hizo zina madeni na zingine zipo chini ya usimamizi au umiliki wa Taasisi nyingine na hivyo kusababisha mashaka kuhusu umiliki wake. Katika hali hii, mali zilizothibitishwa kuwa ni za TLC bila utata zina thamani ya Shilingi 15,952,574,800. Tathmini ilionesha pia kuwa, maveterani walio hai wanahitaji matunzo ikiwa ni pamoja na bima ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati imetoa mapendekezo ya kuuza mali zisizo na utata ambazo nimezitaja za Shilingi 15,952,574,800 na kutoa fidia kwa Maveterani wote walio hai na warithi wa walio fariki. Pia kuwapatia bima ya afya Maveterani walio hai na kuwaenzi Maveterani wote kwa kujenga mnara wa kumbukumbu wa Askari wote waliopigana Vita Kuu ya Pili. Serikali inayafanyia kazi mapendekezo haya na tathmini kuhusu mali zenye utata inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, huu ndiyo mkakati wa Serikali wa kuwaenzi waliopigana Vita ya Pili ya Dunia na kuhakikisha wananufaika na mali zao.