Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 110 2023-09-06

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa Hati kwa maeneo yote ya Umma katika Halmashauri za Mkoa wa Songwe?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri tano za Mkoa wa Songwe, jumla ya maeneo ya umma 1,679 yanatumika kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama vile Shule, Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali, Vyuo, Ofisi, Vituo vya Polisi, Mahakama, Maeneo ya Majeshi, Hifadhi za Misitu na Wanyama na Maeneo ya Makumbusho yanayotumiwa na Serikali au Taasisi. Aidha, maeneo 892 yameshapimwa ambapo kati ya hayo, maeneo 637 yameshakamilishwa na kutolewa Hatimilki.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuongeza kasi ya umilikishaji wa maeneo ya matumizi ya umma, Serikali imefanya jitihada madhubuti ikiwemo kuondoa au kupunguza baadhi ya gharama za umilikishaji wa maeneo hayo. Hata hivyo, baadhi ya Taasisi za Serikali zikiwemo Halmashauri zetu zimeshindwa kutenga fedha katika bajeti zao kwa ajili ya umilikishwaji wa maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa rai kwa viongozi wa Serikali na Wakuu wa Taasisi nchini wakiwemo viongozi wa Halmashauri za Mkoa wa Songwe kuhakikisha wanatenga fedha katika bajeti zao kwa ajili ya kugharamia upimaji na umilikishwaji wa maeneo yao, ahsante.