Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 467 2023-05-30

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASABURI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuubadilisha Mkoa wa Dar es Salaam kwa kujenga barabara za mitaa, mifereji na miundombinu mingine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022 – 2022/2023 Serikali ilitenga shillingi bilioni 100.06 kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara ambapo kilomita 47.77 za lami, kilomita 1,896.966 za matengenezo ya barabara, madaraja na makalvati 70 pamoja na taa za barabara 862. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2023/2024, jumla ya shilingi bilioni 48.68 zimetengwa kwa ajili ya kazi ya barabara katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango uliopo sasa ni wa kuanza utekelezaji wa Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II), pamoja na maboresho ya Mto Msimbazi na Daraja la Jangwani. Miradi hii itahusisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya barabara, mifereji ya maji ya mvua pamoja na madaraja.