Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 468 2023-05-30

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-

Je, lini Mradi wa TACTIC utaanza Singida Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhan Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Singida ni miongoni mwa Miji 45 ambayo imepewa kipaumbele cha kupata ufadhili wa Mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji, Manispaa na Majiji ya Tanzania ambao unaitwa Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness (TACTIC) Project. Ufadhili huu ni wa Serikali Kuu kupitia mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia ambapo unaratibiwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Mradi huu unatekelezwa katika Miji ya Tanzania kwa awamu tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya pili ina Miji 15 ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Singida. Serikali inatarajia kutangaza zabuni za kuwatafuta wasanifu (Design Consultants) mwishoni mwa mwezi Mei, 2023 ambapo wasanifu watakapopatikana wataanza kazi ya usanifu mwanzoni mwa mwaka wa fedha 2023/2024 na ujenzi utaanza mwishoni mwa mwaka wa fedha 2023/2024.