Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 469 2023-05-30

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:-

Je, lini barabara ya Hilbadaw – Bashnet itahamishiwa TANROADS?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007, kifungu cha 11 na Kanuni za Usimamizi wa Barabara ya mwaka 2009 Kifungu 43(1) na (2) na kifungu 44(1) kupitia Tangazo la Serikali Na. 21 ya tarehe 23 Januari, 2009, imeainisha vigezo vya utaratibu wa kuhamisha barabara ili iwe chini ya TANROADS ambapo barabara inaweza kupandishwa au kuteremshwa kutoka daraja moja kwenda daraja lingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na sheria hii, barabara ambayo inakidhi vigezo kutoka daraja la barabara ya Wilaya kwenda daraja la barabara ya Mkoa (kusimamiwa na TANROADS) inatakiwa ijadiliwe kwenye kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa na ikionekana inakidhi vigezo, Bodi hiyo kupitia Mwenyekiti itamshauri Waziri mwenye dhamana na barabara husika, kwamba barabara hiyo imekidhi vigezo na kupandishwa hadhi. Hivyo, nashauri kwamba utaratibu huo uzingatiwe katika kupandisha hadhi barabara ya kutoka Hirbadaw – Bashinet kwenda TANROADS.