Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 470 2023-05-30

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Viongozi wa Serikali ngazi ya Wilaya na Mkoa wanashiriki mafunzo ya JKT ya muda mfupi?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Kujenga Taifa linaendesha mafunzo kwa kundi la lazima (compulsory), kundi la kujitolea (voluntary) na kundi maalum (special). Mafunzo ya kundi maalum hutolewa kulingana na mahitaji yanayowasilishwa na taasisi au Wizara husika na huendeshwa kulingana na maelekezo yanayotolewa na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kuhusu kundi hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu unaotumika katika kuendesha mafunzo ya makundi maalum ni kwa Wizara au taasisi kutuma maombi Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, kisha Jeshi la Kujenga Taifa huelekezwa kuendesha mafunzo hayo, ambapo taasisi ama Wizara husika huyagharamia. Hivyo, endapo kuna uhitaji wa viongozi wa ngazi za wilaya na mikoa kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa kundi maalum, basi Wizara au taasisi inayohusika na viongozi hao iwasilishe maombi hayo ili Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa iweze kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.