Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 471 2023-05-30

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:-

Je, lini Serikali itashawishi mabenki kufungua benki nchini Congo DRC katika Miji ya Kalemie na Uvira ili kurahisisha biashara?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo Mei, 2021 Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania iliipa Benki ya CRDB kibali cha kufungua kampuni tanzu Lubumbashi, nchini Congo ambapo inatarajia kuanza kutoa huduma za kibenki mara tu itakapopewa leseni na Benki Kuu ya nchi hiyo ya Congo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkakati wa Miaka Mitano wa Biashara wa Benki ya CRDB wa mwaka 2023 - 2028 unaonesha kuwa benki hiyo inatarajia kufungua kampuni tanzu zitakazotoa huduma za kibenki kwenye Miji ya Bukavu, Uvira na Kalemie nchini Congo. Hivyo, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano kwa benki za biashara za hapa nchini kuanzisha kampuni tanzu nje ya nchi ili kusambaza huduma za kibenki katika nchi mbalimbali kwa lengo la kurahisisha ufanyaji wa biashara baina ya nchi na nchi, ahsante.