Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 472 2023-05-30

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itarejesha kwa wananchi wa Kata ya Luponde Ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Igeri ambayo kwa miaka mingi imekuwa haitumiki?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haina mpango wa kurejesha shamba la Utafiti wa Kilimo Igeri kwa kuwa kama nchi kuna uhitaji mkubwa wa uzalishaji mbegu. Shamba hilo lina ukubwa wa hekta 816, kati ya hizo, hekta 350 ni misitu ya kiasili, hekta 450 ni eneo linalofaa kwa kilimo na hekta 16 ni eneo lenye barabara na nyumba. Kwa sasa shamba hilo linatumika kwa shughuli za utafiti na kuzalisha mbegu za mazao mbalimbali. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imelima hekta 400 za mbegu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepanga kusafisha, kuweka fensi, kuchimba visima na kulima shamba lote kwa kuzalisha mbegu za awali na za msingi za mazao ya ngano na pareto kwenye hekta 348 na utafiti hekta 88.8. Lengo ni kujitosheleza kwa mbegu za zao la ngano na pareto kwa wakulima wa Njombe, Makete na sehemu nyinginezo. Aidha, natoa rai kwa wananchi kuacha kuvamia mashamba ya utafiti na uzalishaji wa mbegu.