Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 473 2023-05-30

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la ukosefu wa dawa kwa wazee wanaopata huduma ya matibabu bure katika hospitali nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na ukosefu wa dawa kwa wazee, Serikali imeamua dawa ambazo zinatumika sana na wazee zilizokuwa hazitolewi kwenye vituo vya afya na zahanati zianze kutolewa katika ngazi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imewajengea uwezo watumishi wa vituo vya huduma za afya ili kuweza kufanya maoteo halisi kulingana na mahitaji ya dawa ya vituo husika.