Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Water and Irrigation Wizara ya Maji 475 2023-05-30

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa maji Mitaa yote ya Kata za Mbezi Juu, Wazo na Mabwepande katika Jimbo la Kawe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa maeneo ya Kawe, Kata za Mbezi Juu, Wazo na Mabwepande. Hadi kufikia mwezi Desemba, 2022, kazi ya ulazaji wa mtandao wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilometa 391.306 ilikamilika kupitia mradi mkubwa chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi inayoendelea sasa ni ulazaji wa mabomba ya maji umbali wa kilometa 64.3 kuanzia ulipoishia mradi mkubwa kwenda maeneo ya Mpiji Magohe, Mbopo, Mbopo Chekanao na Kinondo na itakamilika mwezi Desemba, 2023.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilika kwa kazi hiyo, maeneo yote katika Kata za Mbezi Juu, Wazo na Mabwepande yatakuwa yamepata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza.