Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 477 2023-05-30

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:-

Je, ni lini Muswada wa Ukomo wa Upelelezi wa Kesi utaletwa ili kupunguza msongamano wa kesi unaotokana na upelelezi kutokamilika?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa kifungu cha 225(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20, ukomo wa upelelezi katika baadhi ya makosa ni siku 60 na kwa mujibu wa kifungu 225(5), Mahakama imepewa mamlaka kuifuta kesi ambayo upelelezi wake haujakamilika baada ya siku 60.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya marekebisho ya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 kupitia Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.1) ya 2022 kwa kuongeza kifungu cha 131A kilichoweka masharti kuwa isipokuwa kwa makosa mazito na makosa yote yanayosikilizwa na Mahakama Kuu watuhumiwa wasifikishwe Mahakamani hadi upelelezi uwe umekalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mkurugenzi wa Mashataka imetoa Waraka Na. 1 wa mwaka 2022, kuhusu Ufunguaji wa Mashtaka na Ukamilishaji wa Upelelezi wa Kesi za jinai uliotolewa tarehe 30 Septemba, 2022 na ulishaanza kutumika tarehe Mosi Oktoba, 2022. Waraka huo unataka upelelezi wa kesi za mauaji, kesi za makosa mazito na kesi zote zinazosikilizwa na Mahakama Kuu ambazo hazihitaji utaalam kutoka taasisi nyingine usichukue zaidi ya siku sitini (60) na zile zinazohitaji utaalam kutoka taasisi nyingine upelelezi usichukue zaidi ya siku tisini (90).