Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 501 2023-06-02

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-

Je, kuna mwongozo unaoruhusu watu wenye ulemavu mmoja mmoja kukopeshwa fedha za Halmashauri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa mtu mwenye ulemavu mmoja mmoja kuweza kupata mkopo ili kujikwamua kiuchumi na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya Taifa. Mwaka 2021 Serikali ilitoa mwongozo wa kumwezesha mtu mmoja mmoja kukopa kwa kufanya maboresho ya Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu za mwaka 2019 za Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, ambapo maboresho hayo yalihusisha kuongeza Kifungu kipya cha 6A(i) na (a) ambacho kwa sasa kinatoa fursa kwa mtu mmoja mmoja mwenye Ulemavu kukopa kutoka katika mikopo inayotolewa na Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge kuendelea kutoa elimu juu ya uwepo wa fursa hii kwa watu wenye ulemavu nchini kwa lengo la kujikwamua kiuchumi na kujiongezea kipato.