Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 504 2023-06-02

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:-

Je, lini Serikali itaboresha Madaraja ya Kampimbi na Mgandu Wilayani Same?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Madaraja ya Kampimbi yapo kwenye Barabara ya Same – Kisiwani hadi Mkomazi yenye urefu wa Kilometa 98. Mkataba kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Same – Kisiwani hadi Mkomazi yenye urefu wa Kilometa 98 umepangwa kusainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023. Ujenzi utajumuisha barabara na madaraja hayo na utaanza katika mwaka wa fedha 2023/2024, ahsante.