Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 505 2023-06-02

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, lini barabara ya Makongolosi – Mkiwa – Chunya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mbeya – Chunya – Makongolosi – Rungwa – Mkiwa (km 503.36) kwa awamu, ambapo sehemu ya Mbeya – Chunya – Makongolosi (kilometa 111) ujenzi umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya Noranga – Itigi – Mkiwa (kilometa 56.9) sehemu ya Noranga – Itigi (Mlongaji) (kilometa 25) umefikia asilimia 12 na kwa sehemu ya Noranga – Doroto (kilometa 6) na Itigi – Mkiwa (kilometa 25.6) mkataba wa ujenzi tayari umesainiwa. Kwa sehemu iliyobaki ya barabara za Makongolosi – Rungwa – Noranga (kilometa 356) na Mbalizi – Makongolosi (kilometa 50) Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi, ahsante.