Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 508 2023-06-02

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, kwa kiasi gani Mkongo wa Taifa umesaidia kuboresha na kupunguza gharama za mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano nchi nzima ambao unafanyika kwa awamu mbalimbali kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, ni kweli uwepo wa muundombinu huu umeboresha huduma za mawasiliano na kusaidia kupunguza gharama za mawasiliano kwa kupunguza gharama za uwekezaji kwa watoa huduma za mawasiliano ambao wangepaswa kujenga muundombinu kama huu kuboresha miundombinu na huduma zao. Hii imesaidia kupunguza gharama za mawasiliano (cost of backhaul transport bandwidth) kwa asilimia 99 na kufanya gharama za maunganisho kwa watoa huduma kupungua kutoka shilingi 157 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi mbili mwaka 2022.

Mheshimiwa Spika, kupungua kwa gharama hizi kumesaidia kushuka kwa gharama za huduma kwa mtumiaji wa mwisho kutoka shilingi 147 kwa dakika mwaka 2009 hadi shilingi 30 kwa dakika mwaka 2022, sawa na asilimia 79.6; hii ni pasipo kutumia vifurushi.

Mheshimiwa Spika, matokeo makuu ya kushuka kwa gharama hizi kupitia miundombinu wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ni kuongezeka kwa matumizi ya huduma za mawasiliano kwa wananchi na Serikali kwa ujumla. Ahsante.