Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 509 2023-06-02

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha matawi ya Vyuo Vikuu vya Umma katika Mkoa wa Katavi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imelenga kupanua na kuboresha huduma za jamii ikiwemo Elimu ya Juu ili kufikia maeneo yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kutokana na azma hiyo, Serikali kupitia Mradi wa Higher Education for Economic Transformation – HEET wa miaka mitano kuanzia mwaka 2021-2026 inatarajia kujenga kampasi mpya 14 za Vyuo Vikuu katika mikoa ambayo haina Taasisi ya Elimu ya Juu ukiwemo Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Spika, Kupitia Mradi wa HEET, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimetengewa jumla ya shilingi bilioni 18.4 kwa ajili ya ujenzi wa kampasi mpya katika Mkoa wa Katavi Wilaya ya Mlele, Halmashauri ya Mpimbwe. Kwa sasa kazi zinazoendelea katika kampasi hiyo ni tathmini ya athari za kimazingira na Jamii yaani environmental and social impact assessment na mchakato wa kumpata mshauri elekezi unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni 2023 na baadaye mkandarasi wa ujenzi, nakushukuru.