Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 512 2023-06-02

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza migogoro ya ardhi maeneo ya Chasimba, Chatembo, Chachui, Nkasangwe na Mabwepande – Kawe?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, migogoro ya ardhi katika Jimbo la Kawe kwa ujumla inahusu wananchi wa Chasimba, Chatembo na Chachui kuvamia eneo la Kiwanda cha Wazo, wananchi kuvamia mashamba ya wananchi wengine katika eneo la Nkasangwe na wananchi kufanya maendelezo katika mashamba yenye miliki likiwemo Shamba la Shirika la DDC katika eneo la Mabwepande.

Mheshimiwa Spika, kwa nyakati tofauti Serikali imekuwa ikishughulikia migogoro hii kwa kuwashawishi wamiliki wa maeneo yaliyovamiwa kuyaachia maeneo hayo ambapo wananchi tayari wameshavamia na kufanya maendelezo na wanapaswa kulipa fidia kwa wamiliki. Hata hivyo, pamoja na jitihada hizo za Serikali kutatua migogoro hiyo kiutawala, kumekuwa na mwitikio mdogo kwa wananchi kulipa fidia kwa maeneo waliyovamia na hivyo kuchelewesha upatikanaji wa suluhisho la kudumu la migogoro hii.