Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 513 2023-06-02

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE K.n.y. MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza:-

Je, Serikali inafanya nini kuhakikisha uviaji mimba usio salama unakwisha?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha uavyaji mimba usio salama unakwisha kama ifuatavyo: -

(i) Kutoa elimu juu ya afya ya uzazi kwa watoto wa kike ambao wapo chini ya umri wa kuzaa, klabu za vijana na vijana balehe kutojihusisha na ngono zembe ili kuepuka kupata mimba zisizotarajiwa.

(ii) Kusimamia utoaji wa huduma za uzazi wa mpango katika vituo vya huduma bila malipo ili kuwawezesha wanawake na wanaume kuzuia mimba zisizotarajiwa.

Mheshimiwa Spika, napenda kuwaasa vijana, akina mama na wanaume wote kwa pamoja wachukue hatua za kuhakikisha kuwa mimba zinazopatikana zinakuwa zimepangwa na wawe wanahudhuria katika kliniki zetu za uzazi wa mpango ili waweze kupatiwa elimu ya afya ya uzazi ikiwemo jinsi ya kuepukana na mimba zisizotarajiwa ili kuondokana na uavyaji wa mimba usio salama, ahsante.