Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 514 2023-06-02

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-

Je, ahadi ya Serikali ya kusambaza umeme wa REA III katika vijiji 48 vya Jimbo la Same Magharibi na vitongoji vyake imefikia wapi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Same, Vijiji 91 kati ya 100 tayari vimepelekewa umeme na vijiji tisa vilivyobaki vitapelekewa umeme ifikapo mwezi Desemba, 2023.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepanga kuanza ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika vitongoji 2,034 nchini kwa gharama ya shilingi bilioni 377.05 ambapo vitongoji 15 katika Jimbo la Same Magharibi vitapelekewa umeme. Serikali itaendelea kupeleka umeme kwenye vitongoji 162 vilivyobaki kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha, nakushukuru.