Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 515 2023-06-02

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Lagana, Itilima na Bunambiyu Wilayani Kishapu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi M/S SUMA JKT anayetekeleza mradi wa REA III Round II katika Wilaya ya Kishapu ana jumla ya vijiji 51 katika mkataba wake, vikiwemo vijiji vya Kata za Lagana, Itilima na Bunambiyu Wilayani. Mkandarasi kwa sasa anaendelea na utekelezaji wa mradi ambapo ameshawasha umeme katika vijiji 13 kati ya 51 sawa na asilimia 25.5. Aidha, kati ya vijiji 13 vilivyowashwa, vijiji vitano ni vya Kata ya Itilima. Mkandarasi anaendelea na ujenzi katika vijiji 38 vilivyobakia vikiwemo vijiji vitano vya Kata ya Lagana, vijiji vitatu vya Kata ya Itilima na vijiji viwili vya Kata ya Bunambiyu ambavyo vinatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2023.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati, Serikali imemfungulia Mkandarasi Hati ya Muamana (LC) ili aweze kuhakikisha anaongeza kasi ya kufanya kazi na kuimaliza mwezi Desemba, 2023, nakushukuru.