Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 534 2023-06-06

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Ikana – Chitete pamoja na kujenga kwa kiwango cha lami barabara za milimani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gelard Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali imetoa shilingi bilioni 1.03 kwa ajili ya matengenezo ya barabara hiyo ambapo miamba ilipasuliwa kwenye kipande chenye urefu wa kilometa mbili ambacho kilikuwa na mwinuko mkali uliokuwa unafanya magari yashindwe kupanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali kupitia TARURA imetenga shilingi milioni 460 kwa ajili ya kuweka tabaka la zege la mita 200, ujenzi wa mifereji na kuongeza upana wa barabara kwa kujaza kifusi kwenye eneo la kona kali.