Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 535 2023-06-06

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuzitangaza ndani na nje ya nchi bidhaa zinazotokana na Zao la Mwani?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Usonge Hamad Juma, Mbunge wa Jimbo la Chaani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitangaza bidhaa za zao la mwani nchini kupitia maonyesho, warsha na matamasha mbalimbali ikiweno Sherehe za Wakulima Nane Nane, Maonesho ya Biashara za Kimataifa Saba Saba, Sherehe za Siku ya Mvuvi Duniani na Siku ya Chakula Duniani. Pia bidhaa za mwani zinatangazwa katika vyombo vya habari mbalimbali ikiwemo runinga, redio, magazeti na mitandao ya kijamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Korea Kusini imeandaa Tamasha la Uvuvi Korea na Afrika (Korea African Fisheries Forum) litakalofanyika Zanzibar kuanzia tarehe 14 hadi 15 Juni, 2023 litakalojumuisha wadau kutoka Korea Kusini na Senegal. Tamasha hili linalenga kutangaza shughuli za uvuvi na ukuzaji viumbe maji za Afrika ikiwemo zao la mwani na bidhaa zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali inaandaa mpango wa kutangaza bidhaa za mwani nje ya nchi kwa kutumia Balozi zetu zilizopo katika nchi mbalimbali kupitia matamasha, vikao na warsha zitakazofanyika katika nchi hizo.