Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 537 2023-06-06

Name

Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:-

Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mahitaji ya nyumba za kuishi Askari Polisi katika eneo la Kengeja Mkoa wa Kusini Pemba. Tathmini kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mbili za makazi ya kuishi familia nne za Askari Polisi imefanyika, ambapo kiasi cha fedha Shilingi 368,412,200/= zinahitajika. Fedha hizo zimetengwa katika Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024, nashukuru.