Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 538 2023-06-06

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:-

Je, ni kwa nini bei ya kuunganisha umeme katika Kijiji cha Lwamgasa ni shilingi 321,000 tofauti na vijiji vingine?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bryceson Magessa Tumaini, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa taarifa kutoka TAMISEMI, eneo la Lwamgasa linatambuliwa kama Mji Mdogo na hivyo malipo ya gharama ya kuunganisha umeme iliwekwa 320,960 kwa vile panakidhi mwonekano wa mji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepokea maombi mengi kutoka kwa wakazi wa maeneo ya vijiji miji wanaotozwa shilingi 320,960 kama gharama za kuunganisha umeme ndani ya mita 30 iwe 27,000. Kijiji cha Lwamgasa ni miongoni mwa vijiji miji hivi. Kwa sasa, uchambuzi bado unaendelea ili kubaini uhalisia wa maeneo hayo. Uchambuzi ukikamilika gharama halisi stahiki zitatolewa, nashukuru.