Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 539 2023-06-06

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, ni kwa nini Wananchi wanaotumia Bima ya Afya wanalalamika kuhusu huduma wanazopatiwa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umekuwa ni nguzo muhimu katika uboreshaji wa huduma za Afya Nchini ambapo Taasisi Binafsi za Afya pamoja na Vituo vya Huduma za Afya vya Serikali vimeonekana kutoweza kujiendesha bila uwepo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kutokana na Watanzania wenye uwezo wa kulipa fedha taslimu kuwa wachache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 70 ya mapato ya vituo vya huduma za Afya vya Serikali pamoja na binafsi vinategemea Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri hayo kumekuwepo na changamoto za kimiongozo ambapo dawa chache zilikuwa zinatolewa katika zahanati na vituo vya Afya. Serikali imefanya maboresho kwa kuongeza idadi ya dawa, vitendanishi na vifaa tiba ambapo kwa ngazi ya zahanati imeongeza kutoka aina 254 hadi 451 na kwa ngazi ya vituo vya Afya toka aina 414 hadi 828.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.