Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 541 2023-06-06

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwakopesha fedha wakulima wa kahawa ili kuondokana na biashara ya butura?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania kwa kushirikiana na taasisi za kifedha ikiwemo Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), imeendelea kuwaunganisha wakulima kupitia Vyama vya Ushirika na kuwapatia mikopo na masharti nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania imeendelea kushirikiana na Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi Ghalani, Soko la Bidhaa Tanzania pamoja na wadau wengine kuweka mfumo rasmi wa masoko na uuzaji wa kahawa za wakulima Mkoani Kagera ili kuwezesha wakulima wa kahawa kupata masoko ya mazao yao.