Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 580 2023-06-12

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itashughulikia kuboresha ujira wa madereva wa magari ya IT?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kutambua mchango wa sekta mbalimbali katika uchumi ikiwemo sekta ya usafirishaji, tayari imepanga kima cha chini cha mshahara kilichoboreshwa ambacho kimeanza kutumika tarehe 1 Januari, 2023. Hivyo mishahara na maslahi kwa madereva imeboreshwa kupitia amri ya kima cha chini cha mshahara kipya.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa kazi kwa madereva wanaoendesha magari ya IT unafanyika kwa kuingia makubaliano ya kazi kati ya mmiliki wa gari na dereva husika ambapo malipo hufanyika baada ya mhusika kufikisha gari linapokwenda. Kwa muktadha huo, mahusiano yaliyopo si ya ajira bali ni makubaliano/mikataba binafsi ya kibiashara (independent contractor) kwa ajili ya contract for service.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, natoa rai kwa madereva wa magari ya IT kuingia mikataba ya kazi ya kibiashara na pale ambapo atatokea mwajiri au kampuni ambayo itaajiri madereva kwa ajili ya kuendesha magari ya IT atapaswa kuzingatia Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ambayo inaelekeza ulipaji wa ujira kulingana na sekta hiyo, ahsante.