Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 582 2023-06-12

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Mjika, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutengeneza barabara zenye hali mbaya katika Mkoa wa Simiyu kila mwaka kutokana na bajeti inayotengwa. Barabara zenye hali mbaya zimeendelea kupungua kutoka kilometa 1,512.71 sawa na asilimia 36.32 mwaka 2020/2021 hadi kilometa 1,126.38 sawa na asilimia 27.05 mwaka 2022/2023. Hii ni baada ya ongezeko la bajeti kutoka shilingi bilioni 5.13 mwaka 2020/2021 hadi shilingi bilioni 18.38 kwa mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga shilingi bilioni 17.78 kwa ajili ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini katika Mkoa wa Simiyu kufanya ujenzi na matengenezo ya barabara za jumla ya kilometa 995.21 ambazo zitapunguza barabara zilizo na hali mbaya kutoka asilimia 27.05 hadi asilimia 19 ya mtandao unaohudumiwa na TARURA.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuzihudumia barabara za Mkoa wa Simiyu kwa kutenga bajeti kwa ajili wa ujenzi na matengenezo ya barabara hizo kulingana na upatikanaji wa fedha.