Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 583 2023-06-12

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tangu Mwaka wa Fedha 2018/2019 hadi mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imeajiri jumla ya Walimu 26,598 wakiwemo 16,640 wa Shule za Msingi na 9,958 wa Shule za Sekondari. Kati ya walimu hao, walimu 1,111 walipangiwa kazi Mkoa wa Tabora na kupelekwa kwenye shule mbalimbali. Kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imeajiri na kuwapangia vituo Walimu 13,130 nchini zikiwemo shule za Mkoa wa Tabora. Kati yao 7,801 ni wa shule za msingi na 5,329 wa shule za sekondari.