Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 585 2023-06-12

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Ofisi za kisasa za Walimu katika kila shule nchini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dorothy George Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Miradi ya Kuboresha Elimu ya Msingi (BOOST) na Sekondari (SEQUIP) imeendelea na azma ya kuboresha Sekta ya Elimu Nchini kwa kujenga shule mpya za msingi na sekondari, ambapo hadi sasa shule 231 za sekondari zimeshajengwa na ndani yake kuna majengo ya utawala ambayo ni ofisi za Walimu za kisasa, vivyo hivyo kwa shule za msingi, shule zote mpya ambazo zinaanza kujengwa, hitaji hili limezingatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Mradi wa BOOST shule nane za zamani zinakarabatiwa sambamba na uboreshaji wa Ofisi za Walimu. Uboreshaji utaendelea kulingana na upatikanaji wa fedha.