Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 587 2023-06-12

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza:-

Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Wilaya ya Uyui - Tabora katika Kata ya Tura na Wilaya ya Ikungi – Singida?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Sekretarieti za Mikoa ya Tabora na Singida imeendelea kutatua mgogoro wa mpaka kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Uyui katika Kata za Tura na Wilaya ya Ikungi. Kamati za Ulinzi na Usalama za pande zote mbili zilikwisha kutana. Kila Mkoa ulipewa majukumu kwa ajili ya kutatua mgogoro huo kwa kufanya yafuatayo:

(i) Wataalam wa Wilaya zote mbili kufika uwandani ili kutafsiri ramani, kufuatilia historia ya eneo, kuandaa kikao cha Majadiliano ya Wataalam na kuandaa kikao cha Wakuu wa Mikoa kuelezea yaliyobainika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wataalam wa Ardhi wa Wilaya ya Ikungi na Wilaya ya Uyui, wanapitia nyaraka mbalimbali yakiwemo matangazo ya Serikali (GN) yaliyoainisha Mikoa hiyo, ramani na mihtasari mbalimbali iliyohusika kupima Vijiji.