Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 590 2023-06-12

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-

Je, Serikali ina mchango gani katika kuboresha huduma za Hospitali ya KCMC ambayo inatoa huduma za afya kwa Kanda ya Kaskazini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeboresha huduma za Hospitali ya KCMC kwa kupeleka fedha za miradi mbalimbali, kulipia mishahara pamoja na ufadhili wa masomo kwa wataalam kama ifuatavyo:-

(i) Serikali inalipa stahiki na mishahara ya watumishi 905 waliopo KCMC ambapo jumla ya shilingi 983,612,500 hutumika kila mwezi.

(ii) Katika Mwaka wa Fedha 2023 Serikali imepeleka kiasi cha shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya dawa, vitendanishi na vifaatiba.

(iii) Katika mwaka wa fedha 2023 Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 5.9 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya hospitali na shilingi milioni 263.6 kwa ajili ya uendeshaji.

(iv) Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetoa ufadhili wa masomo ya ubingwa bobezi kwa watumishi 15 kada ya afya wa KCMC wanaosoma ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.