Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 593 2023-06-12

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaboresha Kivuko cha Kinesi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa miundombinu (jengo la abiria, ofisi, vyoo na uzio) katika Kituo cha Musoma maarufu kama Mwigobero. Mkandarasi amekabidhiwa eneo la ujenzi kwa ajili ya kuanza kazi. Aidha, ujenzi wa miundombinu upande wa Kinesi umepangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2023/2024, ahsante.