Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 617 2023-06-13

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-

Je, kwa nini Vyombo vya Ulinzi na Usalama vilivyopo mpakani mwa Ziwa Tanganyika havina Usafiri wa uhakika?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua mahitaji ya vyombo vya usafiri vya uhakika katika kudhibiti uhalifu maeneo ya mpakani mwa ziwa Tanganyika. Kwa dhamira ya kuimarisha upatikanaji wa usafiri, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kununulia magari na pikipiki ambapo mchakato unaendelea. Pindi yatakapofika, pikipiki na magari hayo yatagawiwa wilaya zote zikiwemo zilizopo mpakani mwa ziwa Tanganyika. Pia katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 4.5 za kununulia boti 10 kwa ajili ya doria baharini na kwenye maziwa. Baada ya kununuliwa, boti hizo zitagawiwa kwenye maeneo yenye changamoto za uhalifu ikiwemo Ziwa Tanganyika, nashukuru.