Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 652 2023-06-19

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya vifaa tiba katika Hospitali za Wilaya zinazojengwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali ilitenga shilingi bilioni 7.1 kwa ajili ya vifaa tiba vya kinywa/meno na macho kwa hospitali 71. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Serikali imetenga shilingi bilioni 15.5 kwa ajili ya vifaa tiba kwenye hospitali 31 zinazoendelea na ujenzi kila moja imetengewa shilingi milioni 500.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba katika hospitali zote nchini ili kuziwezesha kutoa huduma bora kwa wananchi.