Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 655 2023-06-19

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuiwekea SUMA JKT mazingira rafiki ili iweze kukopa na kutekeleza miradi yake kwa wakati?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, SUMA JKT wanaruhusiwa kukopa kwa kuzingatia Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada, Sura 134 kama ilivyo kwa mashirika mengine ya Serikali. Hivyo shirika litatakiwa kuwa na hali nzuri ya kifedha inayothibitisha uwezo wa taasisi kukopa na kulipa.

Mheshimiwa Spika, Mwongozo wa Uandaaji, Utekelezaji na Usimamizi wa Miradi na Majadiliano ya Mikopo, Dhamana na Misaada ya mwaka 2020 umeelekeza hatua muhimu za kuzingatia kwa Wizara au Taasisi ya Serikali ikiwa inaomba mkopo, dhamana na msaada, kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ahsante.