Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 659 2023-06-19

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:-

Je, lini zoezi la kufikisha umeme katika vitongoji, vijiji na mitaa ambayo haina umeme litakamilika Wilayani Kakonko?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili ambapo vijiji vyote visivyokuwa na umeme vitafikiwa na huduma hiyo. Aidha, vijiji saba tu vya Wilaya ya Kakonko visivyokuwa na umeme vitakamilika kuwashiwa umeme ifikapo tarehe 30 Juni, 2023.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha uhakiki wa vitongoji 36,101 visivyo na huduma ya umeme na kuandaa mradi kabambe wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote unaoitwa Hamlet Electrification Project (HEP) vikiwemo vitongoji 196 vya Wilaya ya Kakonko. Mradi huu utatekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2024/2025. Kwa mwaka 2023/2024 Jimbo la Buyungu Wilayani Kakonko litapatiwa fedha kwa ajili ya kupeleka umeme katika vitongoji 15 vya kuanzia, nakushukuru.