Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 660 2023-06-19

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita wanapata mkopo wa elimu ya juu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka hadi mwaka ili kuongeza wigo wa wanufaika. Bajeti ya mikopo iliongezeka kutoka shilingi bilioni 570 mwaka 2021/2022 hadi shilingi bilioni 654 mwaka 2022/2023. Pia mwaka 2022/2023 shilingi bilioni tatu zilitengwa kwa ajili ya Samia Scholarship iliyonufaisha wanafunzi 593 waliohitimu kidato cha sita wenye ufaulu wa juu kwenye masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati.

Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kupanua fursa za mikopo kwa wahitimu wa kidato cha sita, Serikali imeingia mkataba wa mahusiano na Benki ya NMB ili kutoa mikopo yenye riba nafuu ya asilimia tisa kwa wazazi/walezi kwa ajili ya kugharamia elimu ya watoto wao katika ngazi ya elimu ya juu na kati. Aidha, Serikali itaendelea kutafuta fursa za mikopo ya elimu ya juu kutoka kwa wadau mbalimbali ili kuhakikisha kila mhitimu wa kidato cha sita mwenye sifa anapata mkopo kwa ajili ya kugharamia elimu ya juu, nakushukuru.