Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 663 2023-06-19

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kuwawezesha wadau wa michezo kuwekeza katika kuzalisha vipaji vya michezo hasa mpira wa miguu?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, na kwa ridhaa yako, naomba nitumie sekunde chache kuwapongeza vijana wetu wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kwa ushindi wa goli moja kwa bila walioupata dhidi ya Niger jana, ushindi ambao unatuweka katika nafasi nzuri na uwezekano mkubwa wa kuweza kupata nafasi ya kushiriki katika Fainali za Mataifa ya Afrika zitakazochezwa mwakani kule Senegal. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo niliwaahidi jana ile milioni 10 yao ya goli la mama kutoka kwa shabiki na mwezeshaji namba moja wa timu ya Taifa itawafikia leo kwa sababu mama hana kona kona, akishaahidi lazima litekelezwe, ahsante. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum lililoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Abubakari Asenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika kuwezesha wadau kuwekeza kwenye uzalishaji wa vipaji vya michezo hasa mpira wa miguu imefanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuweka miongozo mahususi ya uanzishwaji na uendeleshaji wa shule maalum za kuibua; kukuza na kuendeleza vipaji (sports academies); kuweka mfumo madhubuti wa usajili wa academia na vituo vya michezo; kupunguza kodi kwenye vifaa vya michezo kama vile nyasi bandia na viambata vyake; kutoa utaalamu na ushauri katika ujenzi wa miundombinu ya michezo; na kuandaa mashindano ya UMISETA kwa shule za sekondari na UMITASHUMITA kwa shule za msingi ili kuwashindanisha, kuibua na kuendeleza vipaji vyao, ahsante.