Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Water and Irrigation Wizara ya Maji 757 2023-06-28

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: -

Je, ni wananchi kiasi gani wa Wilaya ya Kyerwa wamefikiwa na huduma ya maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 Wilaya ya Kyerwa ina jumla ya wananchi 368,360 ambapo kati yao wananchi 209,965 sawa na asilimia 57 wananufaika na huduma ya maji kupitia skimu 26 za maji zilizopo. Aidha, katika mwaka fedha 2022/2023 Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji ya Runyinya - Chanya, Nyamiaga – Nyakatera - Kagu, Kimuli - Rwanyango na Chakalisa. Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2023 na kuongeza idadi ya wanufaika kufikia 265,219 sawa na asilimia 72 ya wananchi wa Wilaya ya Kyerwa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itaendelea kuboresha huduma ya maji Wilayani Kyerwa kwa kujenga miradi ya maji mipya ya Kikukuru - Mkunyu, Lubilizi, Businde - Nyakashenye, Bugara pamoja na kukarabati Mradi wa Maji Songembele. Kukamilika kwa miradi hiyo kutawezesha wananchi wote Wilayani Kyerwa kupata huduma ya maji safi, salama na ya kutosheleza. (Makofi)