Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 735 2023-06-27

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari katika Kata ya Mjimwema Makambako?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inatekeleza mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) ambapo ujenzi wa shule mpya unafanyika katika Kata ambazo hazina shule. Katika awamu ya kwanza shule 231 zimejengwa.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi unaendelea ambapo jumla ya shule 1,000 zitajengwa na mchakato wa kupeleka fedha kwa Halmshauri utakapokamilika fedha hizo zitapelekwa. Hivyo, Halmashauri iweke kipaumbele cha ujenzi wa shule hii kwenye mpango wake kwa awamu zijazo katika Kata ambazo hazina shule ikiwemo Kata ya Mjimwema Makambako.