Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 736 2023-06-27

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kutenga fedha ili kuweka uwiano sawa kwa bajeti za Halmashauri kwani Halmashauri nyingi haziwezi kujiendesha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua utofauti uliopo wa uwezo wa Halmashauri kujiendesha baina ya Halmashauri moja na nyingine kutokana na uwezo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri. Kwa kutambua hilo, Serikali imeziweka Halmashauri kwenye madaraja manne kwa kuzingatia uwezo wa Halmashauri kukusanya mapato kutokana na fursa za vyanzo vya mapato vilivyopo kwenye eneo husika la utawala.

Mheshimiwa Spika, ili kuziwezesha Halmashauri zisizo na fursa za kukusanya mapato makubwa kujiendesha na kwa kuzingatia madaraja hayo Serikali imechukua hatua zifuatazo:-

(i) Kuzipunguzia viwango vya upelekaji wa fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo;

(ii) Kuziondolea mchango wa asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa Barabara;

(iii) Kuzisaidia kulipa stahiki za Viongozi hususan Wakurugenzi na Wakuu wa Idara;

(iv) Kuzisaidia kulipa posho za kila mwezi za Waheshimiwa Madiwani; na

(v) Kuziongezea viwango vya ruzuku ya matumizi ya kawaida na ruzuku ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuziwezesha Halmashauri zenye uwezo mdogo wa ukusanyaji wa mapato ili ziweze kujiendesha.