Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Water and Irrigation Wizara ya Maji 739 2023-06-27

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:-

Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa miundombinu ya maji iliyochakaa na kusababisha upungufu wa maji – Chemba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inafahamu changamoto ya uchakavu wa miundombinu ya maji katika Wilaya ya Chemba na imeanza kuchukuwa hatua kwa Vijiji vya Humekwa na Mlongia ambapo manunuzi ya vifaa kwa ajili ya ukarabati yanaendelea. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itafanya usanifu na kufanya ukarabati wa miradi ya maji kwa Vijiji vya Njoeni Muone, Mtakuja, Bugenika, Msera, Mengu, Pangalua, Wahilo, Wisuzaje, Msaada na Mwailanje. (Makofi)