Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 740 2023-06-27

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA aliuliza:-

Je, Serikali imewatafutia eneo mbadala wananchi wa Vijiji vya Kata ya Nyantwari – Bunda wanaofanyiwa uthamini kupitia uhifadhi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Mathew Marwa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali iliamua kutwaa eneo la ghuba ya Speke lenye ukubwa wa ekari 14,250 kwa manufaa ya umma ili kuimarisha uhifadhi endelevu wa mfumo ikolojia wa Hifadhi ya Taifa Serengeti na usalama wa wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, zoezi la uthamini lipo katika hatua za mwisho na baada ya hapo wananchi watalipwa fidia kwa mujibu wa sheria. Fidia itakayolipwa kwa wananachi husika, itahusisha gharama za thamani ya ardhi, mazao, majengo, posho ya kujikimu, usafiri na posho ya usumbufu.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Halmashauri ya Mji wa Bunda imetenga na kupima viwanja 350 katika Eneo la Virian, Kata ya Stoo ambapo wananchi watakaohama kutoka Kata ya Nyantwari watapewa kipaumbele wakati wa uuzaji wa viwanja hivyo.

Mheshimiwa Spika, aidha, Halmashauri ya Mji wa Bunda imeandaa mpango wa kutwaa na kulipa fidia maeneo mbadala ya makazi yenye ukubwa wa ekari 1,625 katika maeneo ya Manyamanyama, Bitaraguru, Butakale na Guta. Maeneo yote hayo yatapimwa na kupewa kipaumbele kwa wananchi wanaotoka Kata ya Nyantwari.