Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 709 2023-06-23

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Mbuguni kuanzia Tengeru Sokoni, Arumeru hadi Mererani utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeanza maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa Barabara ya Tengeru Sokoni – Arumeru hadi Mererani yenye urefu wa kilometa 28 ambapo TANROADS wanaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itakamilika Agosti, 2023. Baada ya usanifu kukamilika Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.