Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 711 2023-06-23

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, Serikali inatumia utaratibu gani kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa Mipango na Bajeti zinazopitishwa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali husimamia na kufuatilia utekelezaji wa mipango na bajeti zinazopitishwa na Bunge kwa utaratibu ufuatao: -

(a) Wizara ya Fedha na Mipango kila mwaka huandaa na kusimamia utekelezaji wa Mwongozo wa Maandalizi na Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Serikali;

(b) Kutoa Waraka Na.1 wa Mwaka wa Fedha wa utekelezaji wa bajeti unaoelekeza na kusisitiza utekelezaji wa vipaumbele;

(c) Kuandaa mwongozo wa maombi na utoaji fedha kwa lengo la kuhakikisha fedha inatolewa wakati wa uhitaji na inatumika kwa wakati;

(d) Kusimamia uwasilishwaji wa taarifa za utekelezaji wa mipango na bajeti na ambazo huchambuliwa ili kutathmini utekelezaji wa mipango kwa kuoanisha na malengo tarajiwa na bajeti zilizotengwa; na

(e) Kubainisha viashiria hatarishi vya utekelezaji wa bajeti na kufanya ufuatiliaji na tathmini ili kujiridhisha na uhalisia na kuchukua hatua stahiki, ahsante.